Serikali imeiagiza Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB), kuwapa wanafunzi 1,107 wenye sifa waliokosa mikopo kwa kutokidhi mahitaji ya Bodi, fursa ya kurekebisha makosa kwa kujaza upya fomu ya maombi ili wapatiwe mikopo.