Kufuatia kichwa cha habari
kilichopo hapo juu, nachukua fursa hii kutoa Historia fupi ya Kijana
huyu anako toka na jinsi ugonjwa alionao ulivyo gundulika mpaka hivi
sasa.
Zuberi Mgeni Zuberi alizaliwa Mwaka
1995 katika Kijiji cha Kwale Kata ya Kwale Wilaya [mpya] ya Mkinga Mkoa
wa Tanga. Alifanikiwa kumaliza Shule ya Msingi kwenye Kata yake hiyo na
akabahatika kuchagulia Mwaka 2010 kuendelea na Masomo ya Sekondari
ambayo ipo kwenye kata hiyo. Lakini hakuweza kuendelea na Masomo hayo
kwa ajili ya Ugonjwa huo. Mwandishi wa habari hii ni Ndugu wa karibu wa
Mama yake Zuberi.
Bado wanaishi pamoja na Baba mzazi wa Zuberi hadi leo na jina lake ndilo hilo Mgeni.
Shughuli wanazo fanya ni Uvuvi na
Ukulima mdogo. Kipato chao ni cha hali ya chini kiasi wali shindwa
kumfanyia uchunguzi Kijana wao ili wafahamu ni kipi kinacho msumbua
Mtoto huyo ambaye mara kwa mara alikuwa akisumbuliwa na Tumbo hivyo
kufikiria kuwa ndiyo Maradhi yanayo msibu, kwahiyo walikuwa wa kimpatia
Dawa za Tumbo ambazo hazikua zikitoa nafuu ya moja kwa moja na ilibidi
awachishwe kundelea na Masomo ya Sekondari ndipo hapo Mwandishi wa
Habari hii ambaye wakti huo alikuwa akiishi Kisiwani Pemba kwa shughuli
za Ujenzi wa Barabara alipo fahamishwa na akatoa msaada wa ushauri na
fedha ili Kijana apelekwe kwenye Hospitali ya Rufaa ya Bombo Mjini Tanga
kwa Uchunguzi na tiba husika Mwaka 2011 Juni.
Hapo ndipo alipo gundulika kuwa
anasumbuliwa na Ugonjwa ndani ya Moyo wake hivyo Hospitali hiyo ikampa
Rufaa ya Kwenda Hospitali ya Taifa ya Mhimbili ambapo amekuwa na Kliniki
hadi leo.
Chakusikitisha nikuwa Madaktari
wa Hospitali hiyo wameshindwa kumpa Rufaa ya kwenda Nchi za nnje kwa
Matibabu kamili baada ya wao kutokuwa na vifaa au ujuzi wa Tiba hiyo,
hivyo ilibidi kutafutwa njia nyengine kwenye Hospitali Binafsi ikiwemo
Regency ambao baada ya utafiti wao wakasema anahitajika kwenda India kwa
Matibabu na Gharama kwa kipindi hicho zilihitajika wastani wa Dola 6000
za Kimarikani sawa na Shs.9,600,000/= za Tanzania.
Zikipatikana anaweza kusafirishwa
na Msaidizi wake mmoja. Maelezo Mengine kwa kina yana weza kupatikana
kwa kuwasiliana na Mwandishi wa Habari hii [Mjomba] moja kwa moja kwa
kutumia Nambari zifuatazo:- 0777 980492 au 0714 980492 Jina lake ni
Bwana Yunus Ally Chui na Mshirika wake wa karibu ni Bwana Feisal Y.
Chui Nambari yake ni 0773 449662.
Msaada wa ki Fedha unaweza kutumwa
kwenye Akaunti zifuatazo: 5753735527 kwa Fedha za Kitanzania na
5753735502 kwa Fedha za Kigeni Bank ya Exim Tawi la Tanga kwa Jina la
Yunus Ally Chui.
Ina ambatanishwa kwenye Barua hii Picha ya Zuberi ili kuthibitisha namna gani Ugonjwa huu ulivyo mbadili Umbile lake.
Ina ambatanishwa kwenye Barua hii Picha ya Zuberi ili kuthibitisha namna gani Ugonjwa huu ulivyo mbadili Umbile lake.
SHUKRAN
No comments:
Post a Comment