Wednesday, 12 June 2013

WATU NANE WASHIKILIWA KUHUSIANA NA KIFO CHA MSICHANA ALIYECHINJWA HUKO MIKOCHENI B

Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam linawashikilia watu wanane, akiwamo mfanyakazi wa ndani anayetuhumiwa kumuua mfanyakazi mwenzake kwa kumchinja.

Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Suleiman Kova, alisema hayo alipozungumza na waandishi wa habari jana.

Alisema Philemon Laiza (27), mkazi wa Mikocheni B, anatuhumiwa kuhusika na mauaji ya Perptua Maina (30) kwa kumchinja na kisha kutelekeza mwili wake kwenye dampo la takataka.

Alisema baada ya polisi kufanya upelelezi mtuhumiwa alikutwa na kiatu kimoja cha marehemu na nguo alizovaa siku ya tukio, ambazo zilikuwa zimetapakaa damu.

Kamishna Kova alisema kuwa mtuhumiwa alipohojiwa alidai kuwa marehemu alitoweka nyumbani tangu siku ya Ijumaa na baada ya kubanwa na polisi mtuhumiwa alikiri kuhusika na tukio hilo

No comments:

 

ADVERTISE WITH US

AFRICAN FASHION

PLACE YOUR ADS HERE!