Wednesday, 12 June 2013

WASANII WENGI WA BONGO HUJISHUGHULISHA NA MADAWA YA KULEVYA, ASEMA JOSEPH MBILINYI "SUGU"

Habari zinaeleza kuwa wasanii mbalimbali nchini, wameingia kwenye mkumbo wa kusafirisha unga tumboni kutokana tamaa ya utajiri na wakati mwingine ni baada ya kuona maisha yao ya kimuziki hayawaendei vizuri. Kutokana na kuingia kwenye biashara hiyo, wasanii hao hususan wanamuziki, hutambuliwa zaidi kwa jina maarufu la punda, kwa tafsiri kwamba wao ni sawa na mnyama huyo ambaye kazi yake kubwa ni kubeba mizigo ya binadamu. Hoja kuhusu jina hilo ni kwamba wanaobeba madawa ya kulevya tumboni, wanajishusha thamani sawa na punda, kwani binadamu ni wale matajiri wanaowabebesha mizigo hiyo.
Joseph Mbilinyi ‘Sugu’. USHUHUDA WA SUGU Ukweli wa jinsi matajiri wauza unga wanavyowatumia wanamuziki wa Kitanzania kama punda, unapewa nguvu na ushuhuda aliowahi kuutoa Mbunge wa Mbeya Mjini (Chadema), Joseph Mbilinyi ‘Sugu’. Mbunge huyo ambaye anapewa heshima kwamba ni mmoja wa waasisi wa Bongo Fleva, alimweleza mwandishi wetu kuwa kabla hajawa memba wa jumba hilo la kutunga sheria, aliwahi kufuatwa na wauza unga kumshawishi awe anabeba mzigo kwenda nao nje ya nchi.    Mwaka 2011, mbunge huyo aliwahi kugusia hilo, wakati akitoa hoja kuchangia bajeti ya Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo kuwa serikali ni lazima iwasaidie wanamuziki wa Kitanzania kwa sababu wanaibiwa sana, hivyo kuwafanya vijana kuona kimbilio rahisi la kutajirika ni kuuza madawa ya kulevya. “Mheshimiwa spika, serikali isifanye ili kijana wa Kitanzania afanikiwe lazima auze unga, madawa ya kulevya,” alisema Sugu na kueleza mfano huo wa jinsi alivyofuatwa kushawishiwa na matajiri wa unga ili naye awe punda.

Source. Fahari ya Mwananchi.

No comments:

 

ADVERTISE WITH US

AFRICAN FASHION

PLACE YOUR ADS HERE!