Friday 20 March 2015

MAELFU WAMZIKA MWANAMUZIKI AK47 NCHINI UGANDA

Jeneza lenye mwili wa AK47 likiwa mbele ya waombolezaji.
MAELFU ya wananchi nchini Uganda jana waliungana na familia, ndugu, jamaa na marafiki kumzika mwanamuziki wa dancehall nchini humo, Emmanuel Mayanja maarufu kwa jina la AK47.


Umati wa watu waliohudhuria mazishi ya AK47 huko Busato nchini Uganda jana.
AK47 alifariki dunia usiku wa kuamkia Machi 17, 2015 baada ya kuanguka akiwa bafuni katika baa iitwayo Dejavu, iliyopo eneo la Kabalagala, Uganda.
Maziko ya AK47 yalifanyika katika eneo la Busato, Wilaya ya Mityana nchini Uganda.
Baadhi ya ndugu na jamaa wa marehemu wakiwa na simanzi wakati wa mazishi ya ndugu yao.
Vilio na simanzi vilitawala eneo la mazishi.
(PICHA ZOTE KWA HISANI YA NEWVISION)

No comments:

 

ADVERTISE WITH US

AFRICAN FASHION

PLACE YOUR ADS HERE!