Friday 4 July 2014

Maendeleo hayana chama – asema Magufuli


DSC_0616
Waziri Wa Ujenzi ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Chato Mheshimiwa Dkt.John MagufuliaAkifurahia na wanachama wapya waliojiunga na Chama cha Mapinduzi CCM katika kata ya Kasenga katika Jimbo la Chato Mkoani Geita.

DSC_0494
Waziri wa Ujenzi ambaye pia ni mbunge wa Chato Mheshimiwa Dkt.John Pombe Magufuli akitoa maelekezo  kwa Mkuu wa wilaya ya  Chato Rodrick Mpogolo wa pili kutoka kushoto pamoja na Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Chato Ndugu Clement Berege (wakwanza kulia). wa kwanza kushoto ni Ndugu Ibrahim Bagura Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Chato.
DSC_0739
Waziri Wa Ujenzi ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Chato Mheshimiwa Dkt.John Magufuli akizungumza na Mkuu wa wilaya ya Chato Rodrick Mpogolo katika ziara yake Kata ya Kachwamba.

Na Mwandishi wetu
Mbunge wa Chato ambaye pia ni Waziri wa Ujenzi Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli amewaasa Wananchi Jimbo la Chato Mkoani Geita kufanya kazi kwa bidii na ushirikiano bila kujali itakadi zao za kisiasa.
Dkt. Magufuli aliyasema hayo jana katika mikutano yake ya kuhamasisha maendeleo katika kata za Kasenga, Ichwankima na Kachwamba wilayani Chato katika mkoa wa Geita.
“Ndugu zangu tufanye kazi kwa bidii, maendeleo hayaji hivi hivi, tuache malumbano na itikadi zetu za vyama ili tujenge jimbo letu vizuri” Alisema Waziri Magufuli
Dkt. Magufuli aliongeza kuwa Serikali ya CCM haina ubaguzi ndio maana inapeleka maendeleo katika maeneo yote na hata yale yanayongozwa na wapinzani.
“Mnatakiwa kushirikiana na Serekali na sio kubeza kama watu wengine wanavyofanya. Serikali yetu imefanya mambo mengi mazuri ya kuwaletea maendeleo” alisisitiza Mheshimiwa Waziri
Katika hatua nyingine Waziri Magufuli alimtaka Mhandisi wa Halmashauri ya Wilaya ya Chato ndugu Peter Ngunula kuhakikisha kuwa ndani ya miezi miwili wananchi wa kata ya Kasenga waanze kupata maji kama awali.
“Mhandisi naomba baada ya miezi miwili wananchi hawa waanze kupata maji kama awali, na wananchi mtunze miundombinu ya maji haya ili tuweze kutatua kero hii kwa pamoja” alisema Waziri Magufuli
Katika kusisitiza jambo hilo Waziri Magufuli alichangia shilingi milioni moja ili zisaidie katika tatizo hilo la maji
Katika hatua nyingine, waziri Magufuli aliwaahidi wakazi hao kuwa Serikali imeanza mchakato wa kuwaletea umeme na wajiandae na fedha kidogo tu Shilingi elfu ishirini na saba 27000/= kwa ajili ya uunganishaji.
Serikali imedhamiria kuwasaidia na kushusha gharama za uunganishaji umeme ndio maana kipindi kile  tunaunganisha umeme pale Chato gharama zilikuwa shilingi laki nne na nusu.

No comments:

 

ADVERTISE WITH US

AFRICAN FASHION

PLACE YOUR ADS HERE!