Thursday 26 January 2017

Ambaka Mama`ke Hadi Kifo

5-002
Marehemu  Fatuma Mohammed Matutu enzi uhai wake.

Dunia imekwisha! Hiyo ndiyo lugha nyepesi na rahisi unayoweza kuitumia kuelezea tukio hili. Januari 11, mwaka huu Tambani, Mbande wilayani Temeke jijini hapa, kijana mdogo, Hamis Lutani Kilumbi (21) anadaiwa kumbaka mama yake mzazi, Fatuma Mohammed Matutu (48) sambamba na kumchoma visu shingoni hali iliyomfanya apate maumivu makali hadi kufariki dunia Januari 21, mwaka huu katika Hospitali ya Taifa Muhimbili.




dsc02127
Kaka wa mtuhumiwa


Akizungumza kwa uchungu na Amani wakati wa mazishi ya mwanamke huyo, mtoto mkubwa wa marehemu aitwaye Mohammed Ali, alisema kuwa siku ya tukio, mtuhumiwa ambaye ni mdogo wake anayemfuata kuzaliwa, alifika nyumbani kwao, alipokuwa akiishi mama yake majira ya mchana lakini hakumkuta.
“Baada ya kumkosa mama, alikuja nyumbani kwangu maana si mbali na anapoishi mama. Lakini pia mimi, mke wangu na mdogo wetu wa mwisho wa kike, Asma, ambaye naishi naye hatukuwepo. Kwa hiyo, Hamis aliacha ujumbe kuwa, tukirudi tupewe taarifa yeye alifika na mama alikuwa anatuhitaji.

dsc02074

Kaka wa Marehemu


UJIO WA MTUHUMIWA WATIA SHAKA
“Sasa baada ya mimi kurudi nyumbani na kupewa taarifa hizo nilishangaa sana, kilichonishangaza si kuitwa na mama bali ujio wa Hamis nyumbani kwangu, maana nilikuwa sijaonana naye kwa muda usiopungua mwaka mzima kwa vile tuliwahi kutofautiana nikampiga marufuku kuja nyumbani kwangu na yeye akaahidi akiniona popote atanipiga na nondo,” alisema Mohammed.

dsc02079

…Mwili wa Marehemu ukitolewa Mochwari
Hata hivyo, Mohammed alisema baada ya kuuliza juu ya wito wa mama yake, aliambiwa kuwa, Asma alishakwenda nyumbani na hakuwa anawaita kama alivyosema Hamis.
Mohammed akaendelea kueleza kuwa, baada ya maelezo hayo, aliamua kuendelea na mambo yake na alikwenda kutazama mechi ya mpira wa miguu kati ya Simba na Yanga runingani zilizokuwa zikicheza Zanzibar.
KWA HISANI YA GPL:

No comments:

 

ADVERTISE WITH US

AFRICAN FASHION

PLACE YOUR ADS HERE!