Wednesday 26 November 2014

WANAWAKE AMBAO HAWAJAOLEWA MARUFUKU KUINGIA KWENYE MIGAHAWA SAUDI ARABIA

Wanawake walio valia mabui mbui nchini saudia.wamiliki wa Migahawa wamewakataza wanawake wasio na waume kuingia katika maeneo hayo.

Migahawa nchini Saudi Arabia imeagizwa kuondoa maelezo yanayowataka wanawake ambao hawana waume kuingia.
Ombi hilo linatoka katika kitengo cha kukabiliana na haki za kibinaadamu ndani ya ufalme wa tafa hilo.
kitengo hicho kinasema kuwa maelezo hayo yanakiuka sheria.
Lakini mmiliki mmoha wa mgahawa amesema kuwa ameweka maelezo hayo kutokana na viwango vya juu vya wanawake wanaotongozwa katika migahawa hiyo.
Tutaondoa maelezo hayo iwapo tutaona kwamba visa kama hivyo havifanyiki tena katika migahawa.
Msemaji wa shirika hilo la kibinaadamu Khalid Al-Fakhri ameliambia gazeti la Saudia kwamba migahawa haina haki ya kisheria ya kuwatenga wanawake ambao hawajaolewa katika maeneo yao ama kusisitiza kwamba wako chini ya mlinzi.
''Haya maelezo yako kinyume na sheria na yanaonyesha maoni yalio na wamiliki wa migahawa hii'',na kuwataka wamiliki hao kubuni mbinu nyengine za kukabiliana na swala la wanawake kutongozwa katika maeneo hayo.
Gazeti hilo pia limemnukuu mwanamke mmoja akisema kuwa ''iwapo watatupiga marufuku kutoingia katika migahawa wanataka twende wapi? Na kuongezea kuwa ni migahawa pekee ambayo wanawake wa Saudia huenda pekee yao.
BBC.

No comments:

 

ADVERTISE WITH US

AFRICAN FASHION

PLACE YOUR ADS HERE!