Friday 22 August 2014

AFRIKA KUSINI WAFUNGA MIPAKA YAKE!

Kila mtu kwao kwa
Nchi ya Africa Kusini inafunga mipaka yake kwa wasafiri kutoka katika nchi za Liberia,Guine na Sierra Leone nchi hizo tatu zimeathiriwa vibaya na mripuko wa ugonjwa wa Ebola


Waziri wa Afya wa taifa hilo, Aaron Motsoaledi,amesema kwamba marufuku hiyo haiwahusu raia wa nchi hiyo ingawa watalazimika kukaguliwa kitabibu ili kubaini endapo watakuwa wamepata uambukizo.
Nao Umoja wa Africa umesema kwamba utaunda timu madhubuti ambayo ni maalumu kwa nchi hizo nne kutoka Africa Magharibi zilizoathiriwa na ugonjwa huo.timu hiyo itahusisha watabibu watakao shirikiana na watabibu wa nchi husika katika kuutokomeza ugonjwa huu.

Pengine haya ni matunda ya ukosoaji wa madaktari wasio na mipaka kuukosoa umoja huo wa mataifa kwa kushindwa kuwajibika kuhusiana na ugonjwa huo.

BBC SWAHILI.

No comments:

 

ADVERTISE WITH US

AFRICAN FASHION

PLACE YOUR ADS HERE!