Thursday 29 May 2014

VIDEO 2 ZA MWISHO ZA MAREHEMU NGWEA KABLA YA KIFO CHAKE HUKO AFRIKA YA KUSINI

Screen Shot 2014-05-28 at 4.37.10 PM
Ngwea Mossred na M2theP
Kila Mtanzania aliemfahamu Ngwea alishtushwa na taarifa za kifo cha Ngwea kilichotokea Johannesburg Afrika Kusini kwa sababu kilikua ni kifo cha ghafla ambapo saa kadhaa baadae nilifanikiwa kuwasili Afrika Kusini na kuanza kuifatilia hii taarifa ambayo bado ilikua inawachanganya kama ni kweli kafariki au sio.

Kwenye hiyo picha hapo juu ni ndani ya dakika 20 tu baada ya kufika kwenye hospitali mwili wa Ngwea ulipokua umehifadhiwa na huyu dada ndio niliongea nae akawa mtu wa kwanza kunipa taarifa kwamba M2theP hakuwa amefariki dunia kama ilivyokua tayari imetangazwa na baadhi ya vituo vikubwa vya TV Tanzania.
Ni mwaka mmoja umetimia leo toka Ngwea afariki dunia ambapo M2TheP kwa sasa amerudi na anaishi nyumbani Tanzania.
Hii hapa chini ni video ya mwisho ambayo Ngwea alionekana siku kadhaa kabla ya kifo chake, alishirikishwa na msanii Mtanzania ambae anaishi Afrika kusini ambae anasema wakati video inafanyika hakukua na ishara yoyote kutoka kwa Ngwea kama angefariki, alikua poa sana.


No comments:

 

ADVERTISE WITH US

AFRICAN FASHION

PLACE YOUR ADS HERE!