Friday 14 March 2014

MADEREVA WA BODABODA NA BAJAJI, WAANDAMANA KUPINGA KUZUIWA KUINGIA KATIKATI YA JIJI DAR..

Madereva Bajaj na bodaboda wakiwa nje ya ofisi za Makao Makuu yaChadema, Kinondoni jijini Dar wakipinga tamko la kuzuiwa kuingia katikati ya jiji.

Polisi wakiwa eneo la tukio kudumisha ulinzi.
 
Mmoja wa madereva Bajaj akiongea na vyombo vya habari nje ya ofisi za Chadema.
 
WAENDESHA bodaboda na Bajaj jijini Dar leo wameandamana mpaka ofisi za Makao Makuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) zilizopo Kinondoni Jijini Dar es Salaam.

 Nia ya maandamano hayo ni kupinga tamko linalowataka kutopeleka abiria maeneo yote ya katikati ya jiji la Dar.

Mmoja wa madereva hao, akiongea na wanahabari alisema kwamba wameamua kuandamana mpaka ofisi za Chadema kwa kuwa wanaamini ndio watapata msaada wa tatizo lao.

No comments:

 

ADVERTISE WITH US

AFRICAN FASHION

PLACE YOUR ADS HERE!