Thursday 23 January 2014

ANA UMRI WA MIAKA 12 AOLEWA KWA NG'OMBE 15

 
Mtoto huyo ambaye jina lake tumelihifadhi kutokana na sababu za kimaadili, hajui kiswahili  vizuri, hivyo nalazimika kumuomba mtoto mwenzake, Stela Paulo aje anisaidie kuongea naye.
Wamasai ni miongoni wa jamii chache duniani, ambazo zimefanikiwa hadi sasa kudumisha mila zake. Katika mila za jamii hii, zipo ambazo zinapaswa kuendelezwa na nyingine zinapaswa kupigwa marufuku.
Miongoni mwa mila ambazo zinapaswa kuendelezwa ni pamoja na kuendelea kutambua na kuheshimu viongozi wa mila ‘Laigwanaji’ kuheshimu viongozi wa rika na Serikali, kuishi kwa umoja na kudumisha tamaduni.
Mila ambazo zimepitwa na wakati katika jamii hii ni pamoja na kurithi wajane, ukeketaji watoto na kuoa watoto wadogo.
Katika makala hii, leo nitazungumzia mila ya kuoa watoto wadogo kama nilivyobaini katika vijiji kadhaa wanapoishi Wamasai, wilayani Kiteto, Mkoa wa Manyara.
Nikiwa katika uchunguzi wa mapigano baina ya wafugaji wa Kimasai na wakulima katika vijiji saba vinavyozunguka eneo la Hifadhi ya Emborey Murtangosi nakutana na mtoto wa miaka 12 aliyeolewa.
Nilipata bahati ya kufika katika familia ya mtoto huyu, katika Kitongoji cha Ndiligishi kaya ya Engusero Sidani baada ya kuwa ni moja ya familia ambazo zimeathirika na mapigano baada ya kuchomewa makazi na kuibiwa vyakula.
Wakati nahojiana na wanafamilia napata fursa ya kuonana na mtoto huyo aliyegeuzwa kuwa mke, nashawishika kumuhoji baada ya kuona akiwa amejitenga na watoto wenzake huku akiwa na mawazo.
Mtoto huyo ambaye jina lake tumelihifadhi kutokana na sababu za kimaadili, hajui kiswahili  vizuri, hivyo nalazimika kumuomba mtoto mwenzake, Stela Paulo aje anisaidie kuongea naye.
Ananieleza kuwa yeye ni mke wa Lembau Leseri  na ameolewa  mke wa pili na ana miaka miwili ya ndoa.
Akiwa  anaonekana kutokuwa na raha ya maisha, mtoto huyo anasema wazazi wake, ndio walimpeleka kwa mwanaume baada ya kupewa mahali.
Anasema hajui kusoma wala kuandika kwani hakufanikiwa kupelekwa shule na wazazi wake.
Ninapomdadisi kama angependa kusoma, anasema angepata fursa hiyo angefurahi lakini sasa haiwezekani tena kwani ni mke mtu.
MWANANCHI.

No comments:

 

ADVERTISE WITH US

AFRICAN FASHION

PLACE YOUR ADS HERE!