Viongozi wa Jubilee nchini Kenya, wameyakosoa mataifa ya Magharibi kwa kuisaliti Kenya na kwamba yamechangia kushindwa kwa hatua ya Umoja wa Afrika ya kulitaka Baraza la Usalama, kuahirisha kesi ya Kenyatta na Ruto.
Viongozi hao wanashtakiwa kwa uhalifu dhidi ya ubinaadamu katika Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu ya ICC, The Hague. Grace Kabogo amezungumza na mchambuzi wa masuala ya kisiasa nchini Kenya, Barack Muluka na kwanza alitaka kujua Jubilee wametumia misingi gani kuzilaumu nchi hizo?
Mwandishi: Grace Patricia Kabogo
SOURCE DW SWAHILI.














No comments:
Post a Comment