Tuesday, 9 July 2013

PENGO KATI YA WALIONACHO NA WASIONACHO LAJADILIWA NA UMOJA WA MATAIFA




Na Mwandishi Maalum
Baraza  Kuu la Umoja wa  Mataifa jana  Jumatatu lilikuwa na  majadiliano    juu ya kukosekana kwa usawa wa kiuchumi na kijamii  kati ya mtu na mtu,   na baina ya nchi na nchi na adhari zake kwa mstakabali  wa amani, usalama na maendeleo endelevu.
Majadiliano  hayo ya siku  moja  yaliandaliwa na Rais wa Baraza Kuu Bw Vuk Jeremic  na kufunguliwa na  Katibu Mkuu Ban Ki Moon, yaliwahusisha   baadhi ya mawaziri kutoka nchi kadhaa, wakuu wa Mashirika yaliyo chini ya Umoja wa Mataifa,  Jumuiya za  Kikanda  pamoja na  Asasi zisizo za kiserikali. 
Akifungua majadiliano hayo, Katibu Mkuu amesema,  licha ya kuwapo kwa mafanikio   kadhaa katika upatikanaji wa huduma  za kijamii, kama vile afya, elimu,  maji safi na  salama  kupitia utekelezaji wa Malengo ya Maendeleo ya Millenia ( MDGs). Bado pengo kati ya walionacho  na wasio nacho ni kubwa na linaendelea kukua.
Kwa mfano, anasema, katika miaka michache  iliyopita jumuiya ya kimataifa imeshuhudia ongezeko la idadi ya  watoto wanaokwenda shule hasa watoto wa kike,  kupungua kwa vifo vya wanawake wajawazito na watoto wachanga, na  vita dhidi ya magonjwa  kama vile malaria,  maambukizi ya ukimwi na kifua kikuu.
 
 
HABARI KWA HISANI YA MICHUZI

No comments:

 

ADVERTISE WITH US

AFRICAN FASHION

PLACE YOUR ADS HERE!