Habari zilizotufikia zinaeleza kuwa wanafunzi wanne
wa chuo kikuu cha Dar es salaam maarufu kwa jina la Chuo cha Mlimani
wamevamiwa na majambazi usiku wa kuamkia leo maeneo ya Yombo chuoni
hapo.
Wanafunzi
hao ambao ni wa mwaka wa nne na wa mwisho wa masomo
walikuwa wamekaa wakijisomea, na ndipo ghafla wakajikuta
wakivamiwa na watu wanne na kuamuliwa watoe komputa zao na pochi za
fedha. Kwa mujibu wa chanzo cha habari hii kutoka chuoni hapo,
wanafunzi hao walikubali kuwapa komputa hizo na pochi za fedha, na
majambazi kuanza safari yao.
Baadaye wanafunzi hao wakawaomba wapate hata nakala ya vitu vyao, na ndipo mmoja wao akaamua kuwafuata na kukumbana na risasi tumboni. Mwanafunzi huyo baada ya kupigwa risasi alianguka chini na kugaagaa chini huku akikosa msaada wa kupelekwa Hospitalini.
Chanzo kimeendelea kusema kuwa wanafunzi wa Chuo hicho waliwasiliana na uongozi ili kupata gari ili wamkimbize mwenzao Hospitalini, lakini ilipita takribani nusu saa hakuna majibu na ndipo walipoamua kujikusanya na kuamua kuwafuata viongozi. Kwa sasa mwanafunzi huyo amekimbizwa Hospitalini kupata matibabu zaidi na mpaka sasa hakuna taarifa yoyote.
Tukio hilo limelaaniwa vikali na UMMA wa chuo kikuu cha Dar es salaam na kuitaka serikali kufuatiliwa na kudhibiti vitendo hivyo vya kikatili chuoni hapo.
Baadaye wanafunzi hao wakawaomba wapate hata nakala ya vitu vyao, na ndipo mmoja wao akaamua kuwafuata na kukumbana na risasi tumboni. Mwanafunzi huyo baada ya kupigwa risasi alianguka chini na kugaagaa chini huku akikosa msaada wa kupelekwa Hospitalini.
Chanzo kimeendelea kusema kuwa wanafunzi wa Chuo hicho waliwasiliana na uongozi ili kupata gari ili wamkimbize mwenzao Hospitalini, lakini ilipita takribani nusu saa hakuna majibu na ndipo walipoamua kujikusanya na kuamua kuwafuata viongozi. Kwa sasa mwanafunzi huyo amekimbizwa Hospitalini kupata matibabu zaidi na mpaka sasa hakuna taarifa yoyote.
Tukio hilo limelaaniwa vikali na UMMA wa chuo kikuu cha Dar es salaam na kuitaka serikali kufuatiliwa na kudhibiti vitendo hivyo vya kikatili chuoni hapo.
Habari na mwandishi wetu SMILE JR MNYAMWEZI.