Mama aibiwa mtoto mchanga akiwa wodini
Neema
Sawaka,
MWANAMKE
mmoja Modesta Sumbuko (26) (pichani) anadaiwa kuibiwa mtoto mchanga wa kiume
katika chumba cha upasuaji alipokuwa akijifungua na watu wasiojulikana katika
Hospitali ya Wilaya ya Kahama Mkoani Shinyanga.
Sumbuko
ambaye ni mkazi wa kijiji cha Butende kata ya Mpunze Wilayani hapa alidai
kuibiwa mtoto wake wa kiume wa siku tatu katika hospitali hiyo akiwa ndani ya
wodi ya wazazi alikokuwa amelazwa baada ya kujifungua kwa njia ya
operesheni.
Akielezea
mkasa huo akiwa katika kitanda chake kwenye wodi ya wazazi, Sumbuko alidai kuwa
mwanaye aliibiwa saa 11 alfajiri wakati akiwa amelala na kwamba baada ya kuamka
aliangalia na kukuta mtoto hayupo.
Wakielezea
tukio hilo wanawake waliokuwa katika wodi hiyo walidai kumwona mwanamke mmoja
ambaye aliingia wodini akiwa amevaa hijabu na ushungi akielekea katika kitanda
cha mwanamke huyo.
Mume wa
mama huyo Emmanuel Matheo alidai kuwa mke wake alimleta katika hospitali hiyo
jumatatu ili ajifungue ambapo kutokana na matatizo alizaa kwa njia ya kufanyiwa
upasuaji.
Kaimu
Mganga Mkuu wa Wilaya hiyo Dk Andrew Emmanuel alikiri na kuthibitisha kuibiwa
kwa mtoto huyo katika wodi ya wazazi alikokuwa amelazwa Sumbuka baada ya
kujifungua.
habari kwa hisani ya Neema Sawaka.
No comments:
Post a Comment