Tuesday 19 December 2017

MAFAHARI WAWILI VUTA NIKUVUTE!

Kama ulifikiri kuwa baby Mama wa Diamond Platnumz, Zari The Boss Lady na Hamisa Mobetto bifu lao limetulia au kuisha kabisa utakuwa umekosea. 

Zari na Hamisa wamekuwa wakiripotiwa kutoelewana na kurushiana vijembe katika mtandao tangu Hamisa alipozaa na Diamond wakati akijua fika Zari na muimbaji huyo wa WCB bado ni wapenzi. Sasa Hamisa na Zari si kwamba wanaviambiana tu kwenye mitandao, bifu lao limeenda mbali zaidi lakini katika njia ambayo ni nzuri. Wakati Zari akitarajia kufanya event yake ya Zari All White Party nchini Uganda nyumbani kwao December 21 mwaka huu, siku hiyo hiyo Hamisa naye ameandaa event yake. Hata hivyo utakumbuka si mara ya kwanza kwa Zari kufanya party kama hiyo nchini Uganda na hata Tanzania ameshafanya hivyo lakini kwa Hamisa ni tofauti kitu ambacho kinatafsiriwa kama bado wanazidizi kuonyeshana umwamba.

No comments:

 

ADVERTISE WITH US

AFRICAN FASHION

PLACE YOUR ADS HERE!