Sunday 30 October 2016

238 wafutiwa matokeo darasa la saba

UFAULU mtihani wa Darasa la Saba umeongezeka kwa asilimia 2.52 kutoka asilimia 67.84 mwaka 2015 hadi kufikia asilimia 70.36 mwaka 2016.

Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani la Taifa (NECTA) Dk Charles Msonde ameyasema hayo leo wakati anatangaza matokeo ya mtihani wa taifa wa Darasa la Saba mwaka 2016.
Amesema, watahiniwa 555,291 kati ya 789,479 waliofanya mtihani huo mwaka huu wamefaulu na watajiunga na kidato cha kwanza 2017.
"Idadi hii ya watahiniwa waliofaulu ni sawa na asilimia 70.36, kati ya hao wasichana ni 283,751 na wavulana 271540. Mwaka 2015 watahiniwa waliofaulu ulikuwa ni asilimia 67.84 kuwa kuwapo ongezeko la ufaulu kwa asilimia 2.52,” amesema Dk Msonde.
Amesema, watahiniwa 16,929 wamepata daraja A, 141,616 wamepata daraja B, watahiniwa 396,746 wamepata daraja C, watahiniwa 212,072 wakipata daraja D na 21,872 wakipata daraja E .
Kwa mujibu wa Msonde, watahiniwa 238 wamefutiwa matokeo ya mtihani huo kutokana na udanganyifu.
Amesema shule 6, waalimu, wamiliki wa shule na wasimamizi wa mitihani wamebainika kufanya udanganyifu na kuwafanyia mtihani wanafunzi.

HABARI LEO.

No comments:

 

ADVERTISE WITH US

AFRICAN FASHION

PLACE YOUR ADS HERE!