Wednesday 20 July 2016

Sh1.6 bilioni husomesha albino 320 kwa mwaka



Mwanza. Shirika la Under the Same Sun linatumia zaidi ya Sh1.6 bilioni kila mwaka kuwahudumia na kuwasomesha wanafunzi 320 wenye ulemavu wa ngozi(albino).

Kutokana na gharama ya kuwasomesha kuanzia elimu ya awali hadi Chuo Kikuu, shirika hilo limeiomba Serikali na wadau wengine kujitokeza kusaidia jukumu hilo ili kuhakikisha albino wanapata huduma zote muhimu za kijamii.
Akizungumza katika ufunguzi wa msimu wa Summer Camp unaoendelea katika viwanja vya michezo vya Chuo cha Ualimu Butimba jijini Mwanza leo, Mkurugenzi wa shirika hilo, Vicky Ntetema amesema shirika hilo hulipa Sh2.5 milioni gharama za masomo kwa mwanafunzi mmoja katika shule binafsi za msingi na sekondari.

No comments:

 

ADVERTISE WITH US

AFRICAN FASHION

PLACE YOUR ADS HERE!