Thursday 4 February 2016

WANAOTUHUMIWA KUMVUA NGUO MTANZANIA WATIWA MBARONI-INDIA

Gari chomwa
Image captionGari la wanafunzi hao liliteketezwa
Wanaume watano wanaotuhumiwa kuhusika katika kumshambulia na kumvua nguo mwanafunzi wa kike mwenye umri wa miaka 21 kutoka Tanzania wamekamatwa, shirika la habari la AP limeripoti.


Ubalozi wa Tanzania nchini humo umeitaka India kuhakikisha usalama wa wanafunzi wote kutoka Afrika wanaosomea nchini India, vyombo vya habari vinasema.
Waziri wa mashauri ya kigeni wa India Sushma Swaraj, aliandika kwenye Twitter kwamba amesikitishwa sana na “kisa hicho cha aibu” kilichotokea Jumapili eneo la Bangalore.
Bi Swaraj amesema polisi wamewakamata washukiwa wanne ambao watafunguliwa mashtaka.
Kamishna wa polisi wa Bangalore N S Megharikh ameambia shirika la habari la AFP kwamba watu watano wamekamatwa kuhusiana na kisa hicho ambacho amesema kinaonekana kusababishwa na “hasira barabarani” na si “ubagusi wa rangi.”
"Tumewakamata watuhumiwa hao watano asubuhi baada ya kuwahoji usiku,” Megharikh ameambia AFP.

No comments:

 

ADVERTISE WITH US

AFRICAN FASHION

PLACE YOUR ADS HERE!