Friday 20 March 2015

WATU 45 WAFARIKI MSIKITINI YEMEN

Baadhi ya jamii za watu waliofariki ndani ya msikiti baada ya milipuko Yemen


Zaidi ya watu 45 wameuawa na wengine wengi kujeruhiwa, baada ya watu wa kujitolea muhanga kujilipua misikitini nchini Yemen.
Watu hao wameuwawa katika milipuko iliyolenga misikiti katika mji mkuu Sanaa wakati wa sala ya Ijumaa.
Milipuko Yemen
Waandishi Habari wanasema kuwa, misikiti yote miwili ni maeneo ya maombi kwa waislamu wengi ambao aaasi wa Ki-Shia, maarufu kwa jina Houthis, wanaodhibiti mji mkuu wa Sanaa.
Kwa miezi kadhaa sasa, kumeshuhudiwa taharuki kubwa kati ya makundi hasimu nchini Yemen, pamoja na makundi yaliyo na uaminifu na mtandao wa Al-Qaeda yaliyo katika maeneo ya kusini na mashariki mwa taifa hilo.

No comments:

 

ADVERTISE WITH US

AFRICAN FASHION

PLACE YOUR ADS HERE!