Wednesday, 7 January 2015

JUISI YA LIMAO

juisi-ya-limao
Juisi ya limao
Naamini kila mtu anajua kutengeneza juisi ya limao, nirahisi sana, kamua maji ya limao,ongeza maji na sukari .lakini je.wajua kutengeneza juisi nzuri yalimao yenye ladha na harufu nzuri ya limao ?ijue njia hii ya uakika.


Kanuni ni hii:
kikombe 1 cha sukari kwa kikombe 1 cha maji kwa  kikombe 1 cha  maji ya limao na kijiko 1 cha chakula cha maganda ya limao.
Siri ya kutengeneza juisi nzuri ya limao nikuanza kwa kuandaa syrup ya sukari (maji ya sukari) . Hii husaidia sukari kuyeyuka vizuri  nakufanya juisi iwe naladha nzuri. Limao  lililoiva hutoa juisi nzuri kuliko limao bichi
Malimao mtini
Malimao mtini
Maitaji
  • Sukari kikombe 1 (unaweza punguza kua ¾ ya kikombe)
  • Kikombe 1 cha maji (kwaajili ya syrup)
  • Kikombe 1 maji ya limao
  • Kijiko 1 cha chakula maganda/majani  machanga ya limao
  • Vikombe 3-4 vya maji baridi (yakuchanganyia)
Njia
1.Osha limao, kwakutumia kisu kikali menya maganda ya juu ya limao  bila ganda jeupe la ndani, pima kijiko kimoja cha chakula.
  • Unawezakuumia majani machanga ya limao ,weka majani sita, Osha majani.
2.Katika sufuria dogo changanya maji kikombe kimoja na maganda/majani ya limao kisha funika na bandika jikoni katika moto mdogo.Yakianza kuchemka ongeza sukari kikombe kimoja, koroga adi sukari yote iyeyuke. Zima jiko ,acha ipoe. (hii ndio syrup ya sukari)
  • Ukichemsha kwa moto mkali maganda yalimao yatafanya maji yawe naladha chungu.
3.Wakati syrup inapoa, Kamua malimao  adi upate kikombe kimoja cha maji ya limao.
4.Changanya maji ya limao na syrup ya sukari,kisha chuja ili kutoa maganda na mbegu za limao.Ongeza  vikombe 3 -4 vya maji baridi ,changanya vizuri ,weka frijini kwa dakika 30 adi 40 ili ipoe.
  • Endapo juisi ni tamu sana,ongeza maji ya limao kidogo.Endapo ni kali sana, ongeza maji baridi adi upate ladha upendayo.
  • Ukiongeza maji mengi sana utapoteza ladha na harufu ya limao
  • Kumbuka malimao hutofautiana ladha ya uchachu kutokana na aina ya mbegu ya limao na pale limao hilo lilipolimwa. Hivyo jali kupata  ladha ya uchachu upendayo wewe
5.Weka vipande vya limao na barafu katika jagi unapotenga .
  • Vipande vya limao si kwaajili ya urembo tu,bali pia huongeza  harufu fresh ya limao kwenye juisi wakati wote.

No comments:

 

ADVERTISE WITH US

AFRICAN FASHION

PLACE YOUR ADS HERE!