Tuesday 4 July 2017

TRA yamwaga ajira 400


Dar es Salaam. Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imetangaza ajira 400 ikiwamo zile zinazohusu maofisa forodha, maofisa kodi na wachambuzi biashara.

Tangazo lililotolewa jana na Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma, limewataka Watanzania wenye sifa kutuma maombi yao kabla ya Julai 17 mwaka huu.
Nafasi nyingine zilizotangazwa ni zile zinazohusu rasilimali watu, wasimamizi wa mifumo ya mawasiliano, wanasheria na wahasibu.
Tangazo hilo limesisitiza kuwa wale wanaohisi kuwa na mahitaji maalumu wanapaswa kujieleza kwenye barua zao ambazo zinawezwa kuandikwa kwa Kiswahili au Kiingereza.
Waombaji wameelekezwa kutuma maombi yao kupitia mtandao wa portal.ajira.go.tz au pia kutembelea mtandao wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma.

No comments:

 

ADVERTISE WITH US

AFRICAN FASHION

PLACE YOUR ADS HERE!