Friday 30 June 2017

TCRA yataka makampuni ya simu kusitisha matangazo yanayowekwa kabla ya miito ya simu

[​IMG]
Mamlaka ya udhibiti wa mawasiliano nchini-TCRA- imeyataka makampuni ya simu kusitisha matangazo ya biashara yanayowekwa kabla ya miito ya simu ili kuwawezesha watumiaji wa simu kupata huduma ya mawasiliano kwa haraka zaidi.

Akizungumza na waandishi wa habari,Mkurugenzi mkuu wa TCRA nchini-TCRA Mhandisi James Mitayakingi Kilaba amesema mamlaka hiyo haiwezi kukubali kuwepo na matangazo ya biashara kabla ya miito ya simu kutoka na kuchelewesha huduma ya mawasiliano ambapo amesisitiza tayari TCRA imeyata makampuni ya simu kukutana kuzungunzia kero hiyo.

Chanzo: ITV

No comments:

 

ADVERTISE WITH US

AFRICAN FASHION

PLACE YOUR ADS HERE!