Wednesday 21 June 2017

KIGWANGALLA: TULIOPINGA WIZI WA MADINI YETU TULIBEZWA,TULIKAMATWA KAMA WEZI

Mbunge wa jimbo la Nzega mkoani Tabora Dkt Hamis Kiwangalla alivyokamatwa wakati wa maandamano ya wachimbaji wadogo machimbo ya Mwashina wilayani Nzega mkoani Tabora,huku wananchi wakikimbia hovyo kwani polisi walitumia mabomu ya machozi na risasi za moto kuwatawanya Tarehe 23.03.2014- Picha ilipigwa na Kadama Malunde wa Malunde1 blog.
******


Kupitia ukurasa wa kijamii wa twitter wa Mbunge wa Nzega Vijijini, Dk. Hamisi Kigwangalla ambaye pia ni Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, ameweka wazi kuwa daima ataendelea kupambana dhidi ya rasilimali za umma, kwani amekuwa mwanaharakati kwa muda mrefu.

“Tuliopinga wizi wa madini yetu tulibezwa, tulikamatwa kama wezi; tuliswekwa ndani, tulionekana wasaliti. Leo kiko wapi? #NasimamaNaRaisWangu” aliandika Dk. Kigwangalla huku watu mbalimbali wakitoa maoni yao.

Kwa mujibu wa Dk. Kigwangalla amebainisha kuwa, suala la kupambana na rasilimali za Taifa alilianza miaka mingi kwani miongoni mwa matukio makubwa ni la Machi 22,2014, ambapo alijitolea kupambana kudai haki  tukio lililopelekea kutiwa nguvuni na Jeshi la Polis

Dk. Kigwangalla anasema  katika kupigania maslai Taifa ataendelea kuunga mkono juhudi za Rais Dk. Magufuli  mwanzo mwisho kwani ni moja ya matunda ya nchi yoyote ile Duniani.

Anasema kiongozi Mkuu lazima alinde na kupigania rasilimali za nchi, hivyo akiwa Mtanzania na kiongozi mwenye dhamana anaunga juhudi hizo bila kuchola.

CRD: MALUNDE BLOG

No comments:

 

ADVERTISE WITH US

AFRICAN FASHION

PLACE YOUR ADS HERE!