Friday 21 October 2016

JOKATE KUIJENGEA UWANJA WA MICHEZO SHULE YA SEKONDARI MAJANI YA CHAI


Jokate Mwegelo akiwasili katika shule ya Sekondari ya Majani Ya Chai ya Vingunguti jijini Dar es Salaam juzi. Kulia kwake ni Mkuu wa shule hiyo, Kasango Pascal Ngozi.

 
 
 
 


Jokate Mwegelo akitoa hotuba yake katika Mahafali ya Nane ya Kidato cha Nne ya Shule ya secondari ya Majani ya Chai. Katika Hotuba yake, Jokate alitoa ahadi ya kuwajengea uwanja wa michezo na matundu ya vyoo shuleni hapo. Ujenzi huo utaanza baadaye.
 
 
 

Mkuu wa Shule ya ya Sekondari ya Majani ya Chai, Kasango Pascal Ngozi akitoa neno la shukrani baada ya ahadi ya Jokate Mwegelo wa kujenga uwanja wa michezo na matundu ya vyoo.
 
 
 

Jokate Mwegelo akimkimkabidhi zawadi ya kuwa mwanamichezo bora wa wanafunzi wa kidato cha nne wa Shule ya Sekondari ya Majani ya Chai, Khalid Ibrahim katika mahafali ya nane ya shule hiyo. 
 


Jokate Mwegelo akimkimkabidhi zawadi mwanafunzi mwenye nidhamu bora kwa kidato cha nne wa Shule ya Sekondari ya Majani ya Chai, Khalid Ibrahim katika mahafali ya nane ya shule hiyo. Anayeshuhudia (kulia) ni mwalimu Mkuu wa Shule hiyo, Kasango Pascal Ngozi. 
 
 


Jokate Mwegelo akiserebuka na wanamuziki wa bongo fleva wanaosoma katika shule ya sekondari ya Majani ya Chai wakati wa Mahafali ya Nane yaliyofanyika juzi. Jokate ameahidi kuijengea shule hiyo uwanja wa michezo na matundu ya vyoo.




Mrembo mwenye vipaji lukuki, Jokate Mwegelo kupitia kampeni yake yake ya kuchangia jamii ijulikanayo kwa jina la “Be Kidotified” ameahidi kujenga uwanja wa michezo kwa shule ya Sekondari ya Majani ya Chai iliyopo Vingunguti jijini.

Akizungumza katika Mahafali ya Nane ya shule hiyo, Jokate alisema kuwa ameguswa na changamoto mbalimbali zinazo ikabili shule hiyo na kuamua kusaidia kwa kupitia kampeni yake hiyo.Tayari Jokate amekabidhi viwanja vya netiboli na mpira wa kikapu kwa shule ya Sekondari ya Wasichana wa Jangwani.

Jokate ambaye alikuwa mgeni rasmi katika mahafali hayo, alisema kuwa serikali peke yake haitaweza kutatua changamoto mbalimbali katika sekta ya elimu na nyinginezo na hivyo inahitaji msaada kutoka kwa sekta binafasi na wadau.

“Nashukuru kwa kunichagua kuwa mgeni rasmi katika mahafali haya, hii imenipa faraja kubwa sana, nimesikia changamoto mbalimbali, kwa kuanzia nitaanza kujenga uwanja wa michezo na matundu ya vyoo,” alisema Jokate.

Alisema kuwa ameamua kuonyesha mfano kupitia ‘Kidoti Brand’ kuchangia maendeleo ya michezo nchini hasa kwa katika shule ambazo ni kiini cha maendeleo ya sekta hiyo hapa nchini. Mbali ya michezo, pia Kidoti Brand inajihusisha zaidi na maendeleo ya elimu hapa nchini.

Mkuu wa Shule hiyo, Kasango Pascal Ngozi alisema kuwa wanalazimika kutumia viwanja vya shule jirani katika kufanikisha masuala ya michezo ambayo ni moja ya masomo muhimu sana.Ngozi alisema kuwa wanatambua kuwa kuna vipaji kibao vya michezo katika shule yao, lakini kutokana na kukosa viwanja bora wameshindwa kuvitambua.

“Tunashukuru Jokate kwa ahadi ya kutujengea uwanja wa michezo na matundu ya vyoo, hii itatoa hamasa kwa wanafunzi wenye vipaji katika michezo mbalimbali kutambuliwa na vile vile kuendelezwa, bado tuna tatizo la jengo la utawala, samani za ofisini na kumalizia uzio wa shule, tunawaomba wadau watusaidie kufanikisha hayo,” alisema Kasango.

Mahafali hayo yalipambwa na burudani mbalimbali za muziki wa bongo fleva, singeli, ngoma kutoka kwa wanafunzi wa shule hiyo.Kati ya wanafunzi zaidi ya 290 wanaomaliza kidato cha nne, Khalid Ibrahim alitwaa tuzo ya mwanamichezo bora huku Latifa Kihiyo akitwaa tuzo ya mwanafunzi mwenye nidhamu.

No comments:

 

ADVERTISE WITH US

AFRICAN FASHION

PLACE YOUR ADS HERE!