Wednesday 17 February 2016

MUSEVENI- NINA IMANI NITASHINDA!

MuseveniImage copyrightYoweri Museveni Facebook
Image captionMuseveni ameongoza Uganda kwa miaka 30
Rais wa Uganda Yoweri Museveni amesema ana imani atashinda urais kwenye uchaguzi mkuu utakaofanyika Alhamisi wiki hii.
Hata hivyo, amesema yuko tayari kukabidhi madaraka kwa mtu mwingine iwapo chama chake kitashindwa.


Akijibu maswali ya mwandishi wa BBC Zuhura Yunus wakati wa kikao na wanahabari ikulu Jumapili, Bw Museveni alisema kwa sasa haoni chama chochote ambacho kinaweza kuondoa chama cha National Resistance Movement (NRM) uongozini.
“Sidhani vyama vya upinzani vitashinda NRM. Kwa sababu tunajua nguvu yetu. Tunajua tutashinda, lakini kama itakuwa tumeshindwa basi tutawaachia wale ambao wameshinda. Lakini sidhani kuna chama kinaweza kushinda NRM wakati huu,” alisema.
Kuhusu kuandaa mtu atakayemrithi muda wake wa kuondoka uongozini ukifika, Bw Museveni alisema hawezi kuandaa mrithi.
“Nimeandaa mrithi kwa shamba langu, lakini sio kwa Uganda. Uganda hawa watu watachagua nani atawaongoza wakati mimi nimestaafu,” alisema.

No comments:

 

ADVERTISE WITH US

AFRICAN FASHION

PLACE YOUR ADS HERE!