Friday 27 November 2015

SERA YA ELIMU BURE INAKARIBIA KUKAMILIKA KUANZA KUTUMIKA JANUARI MWAKANI



Serikali imesema siku za karibuni watatoa muongozo utakaoonyesha jinsi sera mpya ya elimu bure itakavyotekelezwa kuanzia mwezi Januari.




Hii imejulikana baada ya mkutano kati ya Kati Mku wa Wizara ya Elimu, Profesa Sifumi Mchome na wakurugenzi wa Idara tofauti zilizo chini ya wizara hiyo, walijadili kwa kina utekelezaji wa sera kutokana na mikakati iliyowekwa na Serikali ya awamu ya tano.



Katibu wa Wizara ya elimu amesema kuwa mfumo huu mpya utawaletea ahueni wazazi nchi nzima, amesema pia wanategemea kuongeza idadi ya watoto wanaojiunga na elimu ya msingi kutoka asilimia 45 mpaka asilimia 100 itakapofika mwaka 2020.

Elimu bure mpaka kidato cha nne ni ahadi iliyotolewa na Rais Magufuli wakati wa Kampeni.

Akiongelea vyuo vya Ufundi, amesema kuwa serikali ya awamu ya tano imejipanga kuingia kwenye uchumi wa viwanda, kwa hiyo elimu ya ufundi lazima ijielekeze huko.

No comments:

 

ADVERTISE WITH US

AFRICAN FASHION

PLACE YOUR ADS HERE!