Thursday 18 June 2015

MUUAJI WA WATU TISA KANISANI AKAMATWA

Mshukiwa wa mauaji ya watu tisa katika kanisa moja la kihistoria mjini Carolina Kusini amekamatwa.


Kulingana na mwanasheria mkuu Lorreta Lynch,awali maafisa walimtaja kijana huyo wa miaka 21 kuwa Dylann Storm kama mtu waliyekuwa wakimsaka kwa shambulizi la Charleston.
null
Mauaji katika kanisa la kihistoria
Maafisa wa polisi wanasema kuwa mshukiwa huyo aliyejihami na bunduki aliketi katika mkutano wa mafundisho ya biblia kwa takriban saa moja kabla ya kufyatua risasi na kuwaua wanawake sita na wanaume watatu akiwemo mchungaji wa kanisa hilo.
Maafisa wamelitaja shambulizi hilo kama la uhalifu wa chuki.
Bi Lynch amesema idara ya haki itaangazia maswala yote ili kubaini njia mwafaka ya kumfungulia mashtaka mshukiwa.
null
Mauaji
Vyombo vya habari vya Marekani vinasema kuwa bwana Storm alikamatwa huko Selby Carolina kaskazini saa 13 baada ya shambulizi.

No comments:

 

ADVERTISE WITH US

AFRICAN FASHION

PLACE YOUR ADS HERE!