Wednesday, 17 June 2015

MAUAJI YA KUKATWA SHINGO NI TISHIO BUKOBA


Mauaji ya kukata watu makoromeo yaendelea kutikisa Wilaya ya Bukoba, mpaka sasa watu 15 wameshauawa kwa kukatwa shingo kisha kukamuliwa damu.
-Usiku wa kuamkia jana, katika kata ya Nyakato, Bukoba Vijijini, wameuawa watu wawili huku wengine wakijeruhiwa.


  1. Wilaya ya Bukoba (Manispaa ya Bukoba na Bukoba

    Vijijini), Mkoani Kagera, kuna wimbi kubwa sana

    la Mauaji ya watu wasiokuwa na hatia.

    Watu wasiojulikana LAKINI ambao bila shaka

    wanafahamika kwa vyombo vya usalama, wanaua

    watu.

    Toka mwanzoni mwa mwaka huu, watu zaidi ya 15

    wameuawa kwa kukatwa shingo na kuwakamua

    damu.

    Usiku wa kuamkia leo, katika kata ya Nyakato,

    Bukoba Vijijini, wameuawa watu wawili huku

    wengine wakijeruhiwa.

    Wamekatwa shingo, wamekamuliwa damu

    na kutupwa barabarani. Hivi ni kweli kwamba

    Usalama wa nchi yetu umeshindwa kutambua

    na kuwakamata wahusika wa matukio haya?

    Wale waliokamatwa na kisha kuachiwa huru

    nini kinaendelea?? Tunahitaji majibu.

    Tunahitaji ulinzi na usalama wa wananchi

    wenzetu wa Bukoba na nchi nzima.

    Usalama wa Taifa, Polisi, Jeshi, tafadhali '

    okoa maisha ya watanzania wanaouawa bila hatia.

No comments:

 

ADVERTISE WITH US

AFRICAN FASHION

PLACE YOUR ADS HERE!