Friday 26 June 2015

JUST IN .....MAJAMBAZI YAUA ASKARI NA KUPORA FEDHA BENKI YA NMB















WATU wanaodhaniwa kuwa majambazi wamevamia Benki ya NMB tawi la Mkuranga mkoani Pwani na kupora fedha kisha kumuua askari mmoja.


Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani, Jafary Mohamed ameuthibitishia mtandao huu kutokea kwa tukio hilo na kwamba kwa sasa yupo njiani kuelekea eneo la tukio.
"Taarifa hizo nimezipata kuwa watu hao wanaodhaniwa kuwa majambazi kuvamia Benki ya NMB, Mkuranga na kupora fedha ambazo kiasi chake bado hakijafahamika kisha kumuua askari mmoja aliyekuwa nje ya uzio wa eneo hilo la benki ambaye hakuwa kazini ila walinzi wote wa benki wapo salama na silaha zao hazijachukiliwa. Kwa sasa nipo njiani kuelekea eneo la tukio kupata taarifa zaidi." Alisema Kamanda huyo.

No comments:

 

ADVERTISE WITH US

AFRICAN FASHION

PLACE YOUR ADS HERE!