Saturday 30 May 2015

MASHAMBULIZI YA BOKO HARAM YAZIMWA

 Jeshi la Nigeria limezima mashambulizi ya wapiganaji wa kiislamu wa Boko Haram katika mji wa Maiduguri ulioko Kaskazini Mashariki mwa taifa hilo.



Wapiganaji hao wa Kiislamu walikuwa wanafyatua makombora mazito mazito kuelekea mji huo usiku wa kuamkia leo lakini wanajeshi wakahimili mashambulizi na kuwakabili.
Watu 13 wameripotiwa kupoteza maisha yao katika mashambulizi hayo ya Boko Haram.
 Shambulizi limetokea saa chache baada ya kuapishwa kwa rais mpya wa Nigeria Jenerali mstaafu Muhammadu Buhari ambaaye ameahidi kukabiliana na tishio la mashambulizi ya kigaidi ya Boko Haram bila huruma.
Mwandishi wa BBC aliyeko Nigeria anasema kuwa huenda hii ni njia ya kundi hilo la wapiganaji kumuonesha Rais mpya kuwa wangali wapo licha ya mashambulizi makali dhidi yao na majeshi ya muungano wa mataifa ya Magharibi mwa Afrika.
Rais Buhari akihutubia taifa punde baada ya kuapishwa alisema kuwa jeshi la taifa hilo litakita kambi yake katika mji huo wa Maiduguri ilikuitokomeza kabisa kundi hilo la waislamu la Boko Haram.
Awali Katika mahojiano maalumu na BBC, kiongozi huyo mstaafu wa jeshi amesema anatarajia kulishinda kundi hilo baada ya dhamira mpya kutoka jeshini na msaada wa nchi jirani.
"Kwa ushirikiano na majirani zetu Cameroon, Chad, Niger na jumuia ya kimataifa na dhamira ambayo tutapata kutoka katika jeshi, Nafikiri itachukua muda mfupi zaidi kukabiliana nao."

No comments:

 

ADVERTISE WITH US

AFRICAN FASHION

PLACE YOUR ADS HERE!