Sunday 26 April 2015

VURUGU ZAZUKA BURUNDI BAADA YA RAIS NKURUNZINZA KUTEULIWA KUGOMBEA TENA URAIS

Waandamanaji wakiwa Mjini Bujumbura.
Kumezuka ghasia katika Mji wa Bujumbura nchini Burundi kati ya maofisa wa polisi na waandamanaji wanaoishutumu serikali kwa kufanya mapinduzi ya kikatiba.


Waandamanaji walirusha mawe na kuchoma matairi huku maofisa wa polisi wakilazimika kurusha mabomu ya machozi hewani.
Ghasia hizo zinafuatia tangazo la jana kwamba Rais wa Burundi, Pierre Nkurunziza ameteuliwa na chama chake kuwania muhula wa tatu wa urais.
Upinzani umeitaja hatua hiyo kama ukiukaji wa katiba na kuonya kuwa huenda ikaathiri makubuliano ya amani ambayo yalimaliza miaka kadhaa ya mapigano ya kikabila.
Serikali imesema kuwa maandamano hayo si halali.
Maelfu ya raia wa Burundi wamelitoroka taifa hilo katika majuma ya hivi karibuni wakihofia kuongezeka kwa ghasia hizo huku taifa hilo likijiandaa kwa uchaguzi utakaofanyika Mwezi Juni mwaka huu.

CHANZO:GPL

No comments:

 

ADVERTISE WITH US

AFRICAN FASHION

PLACE YOUR ADS HERE!