Wahamiaji 9 walionusurika katika ajali ya boti mbili ziliyozama katika bahari ya Mediterranean, wamewasili katika bandari ya kisiwa cha Lampedusa.
Wahamiaji 300 kutoka Afrika wamekufa maji katika bahari ya Mediterranean, baada ya boti mbili walizokuwemo kuzama maji, Jumatano Februari 1, huku tisa miongoni mwao wakiwa wamenusurika.
Kwa mujibu wa shirika la Umoja wa mataifa linalowahudumia wakimbizi, UNHCR, watu zaidi ya 300 wanasadikiwa kuwa wamekufa maji, iwapo zitaongezwa ajali mbili zilizotokea hivi karibuni. Manusura wameingia katika kisiwa cha Italia cha Lampedusa
No comments:
Post a Comment