Friday 20 February 2015

MSANII MEZ B AFARIKI DUNIA

Msanii Mez B aka Moses aliyekuwa Mkoani Dodoma kwa matibabu baada ya kurudishwa nyumbani na mama yake amefariki Dunia. Mez B alikuwa akiuguliwa na homa ya mapafu [TB] na alikuwa kwenye dozi na leo ilikuwa siku ya tatu toka anatumia dawa hizo. 


Leo asubuhi aliamka na kunywa dawa na chakula ila hali yake haikuwa sawa na kuonekana amelegea. Daktari wake alipigiwa siku na kuamuru awekewe drip ila hali yake ikawa mbaya zaidi, wakati wanampeleka hospitalini alifia walipofika mapokezi. Jirana amelezea haya. 


Pole kwa familia ya Mez B, Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema, Amen

No comments:

 

ADVERTISE WITH US

AFRICAN FASHION

PLACE YOUR ADS HERE!