Baadhi ya picha zikionyesha Jengo la ghorofa tatu la Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) lililopo Mtaa wa Moscow na Libya eneo la Posta Jijini Dar es Salaam linaungua moto.
Moto huo umeteketeza mali kadhaa ambazo bado haijaulikana thamani yake na kutokana na mashuhuda waliokuwepo wakati moto huo ukianza kuwaka wanafikiri moto huo huenda umesababishwa na hitilafu ya umeme lakini msemaji kutoka kikosi cha zima moto amesema chanzo kamili cha moto huo bado hakijajulikana.
Wasamaria wakiliondoa gari lililokuwa karibu na jengo hilo.
Kikosi cha zimamoto na Jeshi la Polisi wakiwa eneo la tukio.
No comments:
Post a Comment