Wednesday 18 February 2015

HALI YA MAMA MZAZI WA MTOTO ALBINO ALIYEUAWA NI MBAYA -MADAKTARI WAZUNGUMZA


Hali ya Esther Jonas, ambaye ni mama mzazi wa mtoto mwenye ulemavu wa ngozi aliyetekwa na kufariki dunia baada ya kukatwa viungo, imeelezwa na madaktari wa hospitali ya rufaa Bugando jijini Mwanza alikolazwa kuwa ni mbaya baada ya kushindwa kupumua kutokana na kuvimba sehemu kubwa ya mwili ikiwamo kichwani.


Mama huyo mwenye umri wa miaka 30 ambaye jana alifanyiwa upasuaji wa kichwa katika hospitali ya rufaa ya Bugando na hali yake  imebadilika ghafla usiku wa kuamkia leo na madaktari wamemuwekea mipira puani kwa ajili ya kumsaidia kupumua ili kuokoa maisha yake.
Mkuu wa kitengo cha dharura katika hospitali hiyo Dk. Derick David amesema kuwa hali ya mama huyo sio nzuri na kwamba kwa sasa anapumua kwa shida na pia hazungumzi na kuongeza kuwa kinachofanyika sasa ni kuendelea kumsafisha vidonda na kumpa antibaotiki ya kukausha vidonda.
Mwenyekiti wa chama cha walemavu wa ngozi mkoani mwanza Alfred Kapole ametoa tamko kuhusiana na tukio hilo.
Mwanamke huyo mkazi wa kijiji cha ilelema wilayani chato mkoani Geita alishambuliwa na watu wasiojulikana na kisha kuporwa mtoto wake mwenye ulemavu wa ngozi – albino aitwaye Yohana Bahati mwenye umri wa mwaka mmoja aliyekuwa amebebwa mgongoni wakati akipika chakula cha usiku.
via>>ITV

No comments:

 

ADVERTISE WITH US

AFRICAN FASHION

PLACE YOUR ADS HERE!