Saturday 15 November 2014

BOKO HARAM WAUDHIBITI MJI WA CHIBOK

Wapiganaji wa kundi la Boko Haram.
Ripoti kutoka kaskazini mashariki mwa Nigeria zinasema kuwa wanamgambo wa Boko Haram wameudhibiti mji wa Chibok , mji ambapo waliwateka nyara zaidi ya wasichana 200 mwezi Aprili.


Wenyeji walisema kuwa wanamgambo hao walivamia mji huo siku ya alhamisi na hadi sasa mji huo uko chini ya udhibiti wao.Seneta mmoja kutoka eno hilo ameiambia BBC kuwa wanajeshi waliokuwa wakiulinda mji huo walitoroka wakati wanamgambo hao walipofanya uvamizi.
wasichana zaidi ya 200 waliotekwa na Boko Haram.
Boko Haram wamekuwa wakiendesha uvamizi kwenye sehemu zilizo karibu na Chibok mara kadhaa tangu wawateke nyara wasichana wengi kutoka shule moja eneo hilo.Tangu wakati huo watu wamekuwa wakilalamika kuwa eneo hilo halijapewa ulinzi wa kutosha.
(Stori: BBC

No comments:

 

ADVERTISE WITH US

AFRICAN FASHION

PLACE YOUR ADS HERE!