Thursday 24 July 2014

MWANARIADHA MAARUFU NCHINI UINGEREZA MO FARAH AMEJIONDOA KUTOKA MASHINDANO YA JUMUIYA YA MADOLA-GLASGOW SCOTLAND


Mo Farah hatoshiriki mashindano ya jumuiya ya madola huko Glasgow
Mwanariadha raia wa Uingereza mwenye asili ya Somalia, Mo Farah amejiondoa kutoka mashindano ya Jumuiya ya Madola mjini Glasgow, Scotland.
Bingwa huyo mara mbili wa Olympiki amejiondoa katika mashindano hayo ya jumuiya ya madola kutokana na ushindwa kupona jeraha lake.

“nimechukua uamuzi huu mgumu wa kujiondoa katika mashindano haya ya commonwealth “amesema mwanariadha huyo wa kikosi cha Uingereza.Hata hivyo ameamua kwendelea kuwepo katika kambi yake ya mazoezi kwa maandalizi ya mashindanoya kuwania ubingwa wa ulaya yatakayofanyika mwezi ujao mjini Zurich.
“Ningependelea kuongeza medali ya commonwealth kwenye medali zangu za ubingwa wa olympiki na ubingwa wa dunia ,lakini mashindano haya yamekuja mapema wakati bado naenndelea kuuguza jeraha na mwili wangu bado haujanikubalia kukimbia”

Mo Farah hatoshiriki mashindano ya jumuiya ya madola huko Glasgow
Wakati huo huo mashindano tayari yameanza,wachezaji wa Judo kutoka nchi za Kenya na Tanzania wapo uwanjani hii leo.
Pia wachezaji wa Table Tennis kutoka Uganda na Kenya wanatupa karata zao katika michuano ya mchujo inayofanyika katika viwanja mbali mbali jijini Glasgow.
Kwingineko, kuna ripoti kuwa wanariadha katika kambi ya kikosi cha Kenya wanasemekana kulalamikia hali duni ya kambi yao.
Baadhi yao wanasema kuwa hawana vifaa vya kimsingi na hali katika kambi hiyo ni mbaya.

Vile vile wamelalamika kuhusu kucheleweshwa kwa marupurupu yao lakini maafisa katika kambi hiyo ya Kenya wamesema masuala hayo ni ya ndani na wanayashughulikia.

No comments:

 

ADVERTISE WITH US

AFRICAN FASHION

PLACE YOUR ADS HERE!