Wednesday 30 July 2014

AJALI YA GARI YAUA BABA NA MWANAYE


Watu wawili, baba na mwanawe, wamekufa baada ya gari walilokuwa wakisafiria kutoka jijini Dar es Salaam kuelekea  Ikwiriri kuacha njia na kugonga kingo ya Mto Kihoi na kupinduka.

Kamanda wa polisi wa Mkoa wa Pwani, Ulrich Matei alisema ajali hiyo ilitokea juzi saa 5:00 usiku, eneo la Kihoi Ikwiriri na aliwataja waliokufa katika ajali hiyo kuwa ni Ramadhani Nassoro aliyekuwa dereva na mwanaye Abuu Ramadhani.
Matei alisema chanzo cha ajali hiyo ni kupasuka kwa tairi. Alisema katika ajali hiyo, Samira Nassoro alivunjika mfupa wa paja la kushoto na alipelekwa Hospitali ya Muhimbili kwa matibabu zaidi.
Kaimu mganga mkuu wa Kituo cha Afya cha Ikwiriri, Edmund Masele alisema maiti zimekabidhiwa kwa ndugu wa marehemu kwa ajili ya maziko.

No comments:

 

ADVERTISE WITH US

AFRICAN FASHION

PLACE YOUR ADS HERE!