Saturday 8 February 2014

UHUSIANO WA KUKOROMA NA UGONJWA WA MOYO

Iwapo utamtikisa au kumgusa hali hiyo hupotea kwa sekunde kadhaa na kama atapata tena usingizi mlio huo hujirudia tena

Si jambo geni kusikia mtu wako wa karibu au mwenza wako anapokuwa amelala kuwa na kawaida akikoroma au kuwa na mikwamo mikwamo ya milio isiyo ya kawaida akiwa katika usingizi mzito.
Iwapo utamtikisa au kumgusa hali hiyo hupotea kwa sekunde kadhaa na kama atapata tena usingizi mlio huo hujirudia tena.
Wengi  wamekuwa wakijiuliza ni kipi husababisha hali ya kukoroma na wengine wamelichukulia kuwa ni suala la kimaumbile kama vile unene lakini sababu hasa wamekuwa hawaijui  lakini kwa upande wa afya linaweza kuwa ni kiashiria cha tatizo la kiafya mwilini.
Tayari kuna tafiti za sayansi ya tiba zinaonyesha mahusiano makubwa ya magonjwa ya moyo na watu wanaokoroma au pingamizi la usingizi.
Watu  wenye pingamizi la usingizi hasa watu wazima wameonyesha kuwa na dalili za  magonjwa ya moyo.
Pingamizi la usingizi ni nini?
Pingamizi la upumuaji usingizini ni hali ya kushindwa kupumua kwa kutumia pua au mdomo kwa muda wa sekunde kumi.
Tatizo hili hutokea zaidi ya mara 30 katika hatua za vipindi viwili ambavyo  kitaalamu hujulikana kama mjongeo wa kasi wa macho na mjongea wa kawaida wa macho.
 Mjongeo wa kasi wa macho wakati wa usingizi ni kipindi kimojawapo cha usingizi wa kawaida ambacho huambatana na macho kucheza cheza yaani mtu anakuwa yupo usingizini huku macho yake yakicheza cheza.
Kwa kawaida wakati mtu amelala hupitia hatua hii mojawapo ya usingizi na hutokea mara nne hadi tano katika usingizi.
Hali hii huweza kutokea kwa muda mfupi  na  mwishowe kipindi hiki hukawia kwa muda mrefu hasa inapokaribia asubuhi. Inakisiwa kuwa mjongeo wa kasi wa macho huchukua asilimia 20-25 ya usingizi wa mtu mzima yaani dakika 90-120 kwa ujumla.
Katika hali ya mjongeo wa kawaida wa macho ni hatua ambayo mtu anakuwa amelala lakini  hawezi kuchezesha macho, kuota ndoto ni nadra sana kwa wenye kupata hatua hii. Akili huwa katika hali njema kabisa viungo vya mwili wake kutolegea ndio maana mtu anaweza kutembea huku akiwa usingizini. (sleep walk

No comments:

 

ADVERTISE WITH US

AFRICAN FASHION

PLACE YOUR ADS HERE!