Katiba Mpya ya Kenya imeanzisha mambo mengi mapya. Imeshusha madaraka kwa wananchi na kuwapa madaraka makubwa magavana ya kuamua mambo mbalimbali.
Kenya ilizindua Katiba mpya Agosti 27 mwaka 2010 kwenye sherehe iliyojaa mbwembwe katika bustani ya Uhuru, Nairobi.
Hiyo ilikuwa baada ya Wakenya kupiga kura kwa wingi wakiunga mkono Katiba Mpya. Badala yake katiba imekuwa chungu kwa Wakenya kwa magavana kuaanzisha ushuru wa aina mbalimbali ikiwemo ushuru wa kuaga maiti.
Inatafsiriwa kuwa, magavana wametumia mamlaka yao kunyanyasa wananchi katika kaunti.
Katika Kaunti ya Kiambu, inayoongozwa na Gavana William Kabogo, kuna ushuru mpya unaotozwa kwa familia iliyopoteza mpendwa ama wapendwa wao.
Hakuna anayekubaliwa kumzika mfu wao bila kulipa ushuru huo. Pia, huwezi kuchinja mfugo wako nyumbani bila kulipa ushuru!
Katika Kaunti ya Kakamega, Gavana amebuni ushuru wa kuku ambapo kila mfugaji atalipa Sh20 kwa kila kuku anayemfuga.
Pia, watu wanapoomboleza, lazima walipe ushuru wa kuomboleza haswa wanapotazama mwili wa marehemu.
Ukiutazama zaidi ya mara mbili, utalipa ushuru zaidi ya mara moja!
Watu hawajui la kufanya na wana majuto makuu kwa kukaribisha Katiba mpya 2010. Walipokuwa wanaipitisha walikuwa na matumaini kwamba ingebadilisha maisha yao kwa kuleta utawala na huduma za Serikali Kuu karibu yao.
Wakati huo wa mchakato wa Katiba mpya, Makamu wa Rais William Ruto alikuwa katika upande uliokuwa ukipinga Katiba hiyo.
Kutetea Katiba
MWANANCHI..
MWANANCHI..













No comments:
Post a Comment