Picha na silivan Kiwale
Mkurugenzi wa zamani wa Fedha wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT),
Elisa Issangya, akiwa ameduwaa baada ya vyombo vyake kutolewa
nje ya nyumba na Kampuni ya Udalali ya Mwafrika.
Dar es Salaam. Mkurugenzi wa zamani wa Fedha wa Benki
Dar es Salaam. Mkurugenzi wa zamani wa Fedha wa Benki
Kuu Tanzania (BoT), Elisa Issangya amejikuta akitupiwa vyombo
vyake nje na Kampuni ya Udalali ya Mwafrika kwa kile kilichoelezwa
kutakiwa kuondoka kwenye nyumba aliyokuwa akiishi.
Nyumba hiyo iliyoko Mtaa wa Ruhinde Block 2 Plot 294 eneo
Nyumba hiyo iliyoko Mtaa wa Ruhinde Block 2 Plot 294 eneo
la Ada Estate wilayani Kinondoni jijini Dar es Salaam, inaelezwa
kuwa inamilikiwa na BoT.
Akizungumza nyumbani kwake baada ya kutupiwa nje vifaa vyake
Akizungumza nyumbani kwake baada ya kutupiwa nje vifaa vyake
Issangya alisema: “Nimeshtukizwa na maofisa wa Kampuni ya Udalali
ya Mwafrika kuingia ndani kwangu na kuniomba nishirikiane nao kutoa
vitu vyangu nje.
“Maofisa hao wa Kampuni ya Mwafrika walifika nyumbani kwangu
“Maofisa hao wa Kampuni ya Mwafrika walifika nyumbani kwangu
asubuhi na kunionyesha barua kutoka BoT ya kunitaka kuvitoa vyombo
vyangu nje, sikukubaliana nao, nikaamua kwenda polisi kutoa
taarifa,” alisema.
Alisema wakiwa polisi na ofisa mmoja wa kampuni hiyo aliyemtaja
Alisema wakiwa polisi na ofisa mmoja wa kampuni hiyo aliyemtaja
kwa jina moja la Gama ambaye alikuwa akimweleza kuwa
watamuelewesha
suala hilo baada ya kuondoa vyombo hivyo , lakini waliporejea nyumbani
kwake, walikuta vyombo vyote vimetupwa nje.
Issangya alisema kitendo cha kutupiwa vifaa nje ni udhalilishaji kwani
Issangya alisema kitendo cha kutupiwa vifaa nje ni udhalilishaji kwani
walitakiwa kwenda nyumbani kwake wakiwa na barua ya mahakama
ya kuwaruhusu kufanya hivyo.
“Nimeshangaa hatua hiyo wakati mpaka sasa kesi yangu ya kudai
“Nimeshangaa hatua hiyo wakati mpaka sasa kesi yangu ya kudai
haki zangu ipo mahakamani, wangesubiri mpaka hukumu ikitolewa
ndipo waje na uamuzi huu,” alilalamika Issangya aliyeteuliwa kushika
nafasi ya Mkurugenzi wa Fedha wa BoT mwaka 2000 kabla
ya kusimamishwa 2008.
Alipoulzwa sababu za kufanya hivyo wakati suala la mlalamikaji bado
Alipoulzwa sababu za kufanya hivyo wakati suala la mlalamikaji bado
liko katika vyombo vya sheria na uamuzi wa shauri haujafikiwa
Ofisa wa Kampuni hiyo ya Udalali, Joseph Gama alisema kuwa
wanatekeleza maagizo ya tajiri wao na si vinginevyo.
“Sisi tunafanya kazi kwa amri ya tajiri wetu, hatuwezi kufanya mambo
“Sisi tunafanya kazi kwa amri ya tajiri wetu, hatuwezi kufanya mambo
kinyume na maelekezo, tumeelekezwa na huu ni utekelezaji wake,” alisema
No comments:
Post a Comment