Wednesday 22 January 2014

UMEONA HII DHARAU? MWANAMKE WA RUSSIA HIKI NI KITI CHENYE UMBO LA MWANAMKE WA KIAFRIKA..

Russian Socialite ambae ni muhariri wa jarida la Garage magazine, Dasha Zhukova akiwa pia ni patner wa mmiliki wa club ya Chelsea Roman Abramovich, ameingia kwenye maporomoko ya matusi na maoni mengine mazito ya watu mbalimbali mtandaoni baada ya kusambaa kwa picha inayomuonyesha akiwa
amekaa kwenye kiti kilichotengenezwa kwa mfano wa Mwanamke wa Kiafrika.
Mwanamke huyu ambae anasema ana mapenzi na fashion pamoja na usanii wa vitu kama hivi amekosolewa na wengi ambapo baadhi ya Wanawake hata wenye ngozi kama ya Dasha, wamemkosoa huku wengine wakiuliza ‘bado tunafanya vitu hivi mpaka huu mwaka wa 2014?’
Screen Shot 2014-01-22 at 9.38.20 AM
Kiti hiki kimedizainiwa na msanii raia wa Norway Bjarne Melgaard ambapo baada ya kupostiwa kwa picha hii kwenye mitandao akiwa anafanyiwa interview na tovuti ya Buro 24/7 , muda mfupi baadae waliitoa hii picha na kuomba radhi kwa kitendo hicho

No comments:

 

ADVERTISE WITH US

AFRICAN FASHION

PLACE YOUR ADS HERE!