Friday 31 January 2014

MTANGAZAJI WA TELEVISHENI YA EAST AFRICA(EATV),KEN KIDAGO AFARIKI DUNIA

Mtangazaji wa Kituo cha Televisheni cha East Africa aliyekuwa akifanya kipindi cha 5 sports, Ken Kidago amefariki dunia.
Taarifa ambazo pia zimethibitishwa na mmoja wa wafanyakazi wa kituo hicho zinaeleza kuwa tangu jana januari 30,2014 Ken hakuonekana kazini ambapo simu zake zilikuwa zikipigwa bila majibu ikabidi uongozi wa EATV kutoa taarifa kwa jeshi la polisi nchini Tanzania,walipofika nyumbani kwake Mlalakua jijini Dar es salaam wakagonga mlango hakufungua kabidi wavunje na kuingia na kukuta amefariki.

Taarifa zinaeleza kuwa Jeshi la Polisi linaendelea na uchunguzi wa sababu ya kifo chake.

Ken Kidago aliwahi kuwa mtangazaji wa Radio Ukweli ya mjini Morogoro kabla ya kwenda Arusha ambapo alirejea jijini Dar es salaam hivi karibuni na kujiunga na East Africa Television


CREDIT UDAKU SPECIALLY.

No comments:

 

ADVERTISE WITH US

AFRICAN FASHION

PLACE YOUR ADS HERE!