
Polisi akiwa analinda makasha yenye dawa za kulevya yaliyoingizwa
nchini Ujerumani kutoka Columbia kwa kuwekwa ndani ya ndizi

Polisi akifungua moja ya nizi ambazo ndani yake kuliwekwa dawa za kulevya
Mjini Berlin huko Ujerumani kwenye Supermarket zipatazo tano yamepatikana makasha yaliyojaa ndizi ambamo ndani yake kulikuwa na dawa za kulevya zilizofichwa zinazokadiriwa kuwa na uzito wa kilo mia moja arobaini.
Uchunguzi wa awali unaonyesha kuwa huu ni mtindo ambao umekuwa unatumiwa na wasafirishaji wa madawa ya kulevya. Hata hivyo safari hii kulifanyika makosa ya mawasiliano ambapo mpokeani alianza kuyasambaza makasha hayo kwenye Super Markets akidhaniwa kuwa ni ndizi.
Makasha ya kwanza yalifikishwa kwa muuza matunda kwa jumla kwenye mji hamburg baada ya kuwasili kwa meli kutokea Colombia ikiaminika kuwa ni ndizi.
Wafanyakazi wa hizi Supermarket ndio walitambua kuwa makasha ambayo ndani yake ndio kulikuwa na hizo kilo 140 za unga aina ya Cocaine saa kadhaa baada ya ndizi kuanza kuuzwa kwenye maduka yao.
Makasha ya kwanza yalifikishwa kwa muuza matunda kwa jumla kwenye mji hamburg baada ya kuwasili kwa meli kutokea Colombia ikiaminika kuwa ni ndizi.
Wafanyakazi wa hizi Supermarket ndio walitambua kuwa makasha ambayo ndani yake ndio kulikuwa na hizo kilo 140 za unga aina ya Cocaine saa kadhaa baada ya ndizi kuanza kuuzwa kwenye maduka yao.
CREDIT ..DAR 24













No comments:
Post a Comment