Washiriki waliohudhuria sherehe za uzinduzi wa mwongozo mpya wa huduma za kuzuia maambukizi ya virusi vya ukimwi kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto wakisikiliza na kushangilia hotuba ya uzinduzi iliyokuwa ikitolewa na Mke wa Rais Mama Salma Kikwete aliyekuwa Mgeni rasmi kwenye uzinduzi huo uliofanyika kwenye ukumbi wa Mwalimu Nyerere tarehe 22.1.2014.
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akizindua rasmi mwongozo mpya wa huduma za kuzuia maambukizi ya virusi vya ukimwi kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto, (PMTCT OPTION B+) kwa Mkoa wa Dar es Salaam katika sherehe iliyofanyika katika ukumbi wa Mwalimu Nyerere tarehe 22.1.2014.Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akiwasalimia wazazi wa mtoto Debora Andrew (aliyembeba) , mwenye umri wa miezi 9, ambaye hana maambukizi ya VVU kutoka kwa wazazi wake wanaoishi na virusi vya ukimwi ambao hutumia dawa za kuzuia maambukizi kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto. Mama Salma alikutana na wanafamilia hao wakati wa uzinduzi wa mwongozo mpya wa huduma za kuzuia maambukizi kwa Mkoa wa Dar es Salaam uliofanyika kwenye Ukumbi wa Mwalimu Nyerere tarehe 22.1.2014.
No comments:
Post a Comment