Saturday, 23 November 2013

CHRISTINE AELEZA KISA CHA MAUAJI YA MAPENZI DSM



Dar es SalaamImebainika kwamba sababu ya shambulizi la risasi lililotokea

 Ilala Bungoni, Dar es Salaam Jumanne iliyopita
 na kusababisha vifo vya watu watatu, ni wivu wa mapenzi uliopindukia.
Akizungumza nyumbani kwao Ilala Bungoni jana, mmoja wa majeruhi 

ambaye ndiye aliyekuwa kiini cha shambulizi hilo
 Christine Newa alisema si kweli kwamba sababu ya mchumba wake

 Gabriel Munisi kuwashambulia na kuwajeruhi
 kwa risasi yeye na mama yake mzazi, Ellen Eliezer na kumuua mdogo

 wake wa kike, Alpha Newa ni kutokana na kusaliti
 uchumba wao.
Awali, ilidaiwa kwamba sababu ya shambulizi hilo ni Christine kumkataa

 Munisi, (ambaye pia alijiua baada ya kufanya
mauaji hayo) na kuchumbiwa na rubani wa ndege, marehemu Francis Shumila

 ambaye pia alifariki katika tukio hilo.
.. “Kwanza Shumila hakuwa mchumba wangu kama ilivyoelezwa.

 Alikuwa shemeji yangu, mume wa dada yangu Caroline Newa.
 Pia hakuwa rubani wa ndege, bali nahodha wa meli.”
Alisema amekuwa katika uhusiano wa kimapenzi na Munisi katika kipindi

 kisichofikia mwaka mmoja lakini sehemu
kubwa ya maisha yao ikitawaliwa na misuguano iliyowafikisha polisimara kadhaa.
Alisema katika kipindi cha uhusiano wao marehemu Munisi alikuwa 

akimpiga, akimkataza kufanya kazi, kusoma
na alikuwa na wivu uliopindukia.
Christine kuona hivyo, aliamua kufanya mipango ya kwenda kusoma

 katika Visiwa vya Cypruskimyakimya pasi
 na kumuaga, jambo ambalo alisema lilimkera mchumba wake huyo na kuweka

 kisasi.
“Nikiwa huko, Munisi alitafuta mawasiliano hadi akayapata 

na tukawasiliana.

 na siku niliporejea alikuja kunipokea
 uwanja wa ndege lakini cha ajabu, alinikataza kwenda nyumbani na badala yake akanipeleka moja kwa moja hadi Mwanza
 eneo la Kitangiri,” alisema na kuongeza: “Tukiwa njiani kuelekea

 Mwanza, katika maeneo ya Singida,
 alisimamisha gari akaniambia nishuke, akatoa bastola na kuniuliza

 kwa nini niliondoka bila ya kumuaga. Je, nataka kumuacha?”
Alisema alimwomba msamaha na kuendelea na safari yao. Anasimulia

 kwamba baada ya kufika Mwanza, alimpora simu zake zote
 na kumfungia ndani kwa zaidi ya wiki mbili hadi alipopanda kwenye

 dirisha na kuomba msaada kwa majirani
 na kuwapa namba za simu za ndugu zake ili wamsaidie kuwapa taarifa.
Ndugu zake walianza mchakato wa kuwasiliana na polisi hatua iliyofanikisha

 msichana huyo kurudishwa Dar es Salaam...
 “Hata hivyo niliondoka na khanga na fulana tu. Vitu vyote niliviacha huko.”
Baada ya kurudi Dar es Salaam, anasema Munisi naye aliamua kumfuata

 lakini safari hii alifikia katika Hoteli ya MM iliyotenganishwa na ukuta

 wa nyumba yao na akawa anafuatilia nyendo za familia hiyo.
“Alikuwa ananitumia meseji kwamba amemuona dada Caro, mama na Alpha

 na wakati mwingine anasema ameniona mimi mpaka nguo tulizovaa, tukaanza

 kupata na wasiwasi,” alisema.
Wasiwasi huo ulitokana na historia ya maisha yao ya Mwanza na pia tishio ambalo 

anadai kwamba Munisi aliwahi
 kulitoa kwamba atahakikisha anaiteketeza familia yote kuanzia Goba anakoishi

 mama yake (Ellen), Zanzibar anakoishi
 mdogo wake (marehemu Alpha) na hapo Ilala.
Anasema walikwenda polisi lakini walielezwa kwamba hayo ni masuala madogo ya mapenzi

 na kwamba yatamalizwa kifamilia.
Siku ya tukio Christine alikuwa akitoka kwenda uwanja wa ndege tayari kwa safari

 ya kurudi shuleni Cyprus
ndipo Munisi alipotokea na kuanza kumrushia Shumila risasi na baadaye Alpha

 kisha mama na yeye kabla ya kujiua.
Akizungumzia tukio hilo, Caroline alisema mumewe alitabiri kifo chake kabla kwani baada

 ya kusikia vitisho vya Munisi
, alimtoa shaka Christine akimwambia kwamba atamlinda hata ikibidi kupoteza maisha yake, jambo ambalo lilidhihiri.
Alisema mama yake amepata nafuu na ameruhusiwa kutoka katika Hospitali ya Taifa

 Muhimbili alikokuwa amelazwa na mazishi ya mdogo wake, Alpha ambaye ameacha

 mtoto mwenye umri wa miezi minane, yamepangwa kufanyika Jumamosi

 Goba, Dar es Salaam.
Alisema mipango ya mazishi ya mumewe inafanywa huku akidokeza kwamba huenda

 akasafirishwa kwenda Mombasa.
chanzo:mwananchi

No comments:

 

ADVERTISE WITH US

AFRICAN FASHION

PLACE YOUR ADS HERE!