Wachezaji wawili wa Ivory
Coast wametimuliwa kwenye kikosi kinachojiandaa na mchezo kuwania kufuzu
michuano ya kombe la dunia mwaka 2014 dhidi ya Tanzania unaotarajiwa kupigwa
uwanja wa Taifa siku ya Jumapili.
Mchezaji wa zamani wa
Monaco Jean-Jacques Gosso Gosso, 30, ambaye kwa sasa anacheza kwenye ligi ya
Uturuki akiichezea Mersin na kinda la miaka 20 Abdul Razack wa Manchester City,
ambaye kwa sasa yupo kwa mkopo Charlton Athletic, walipigana siku ya jumatano
wakati timu yao ikiwa kwenye maandalizi ya mwisho kabla ya kuelekea Tanzania .














No comments:
Post a Comment