Friday, 7 June 2013

SPIKA WA BUNGE MAKINDA AWATOLEA UVIVU WABUNGE WAPENDA VIJEMBE





Spika wa Bunge Anne Makinda juzi alikemea tabia ya baadhi ya wabunge na Mawaziri kutumia dakika zao vibaya badala ya kuchangia hotuba wanatumia muda huo kuwashambulia wenzao.

Makinda alitoa kauli hiyo juzi wakati akiahirisha kikao jioni muda mfupi baada ya Bunge kupitisha Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi.Katika hotuba hiyo, wabunge wa upinzani walikuwa wakielekeza michango yao kwa Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Dk Shukuru Kawambwa wakimtaka ajiuzulu.

Makinda alisema kuwa tabia hiyo ni kero kubwa kiasi cha kufanya wananchi waone kuwa Bunge ni sehemu ya malumbano na vijembe. Hii sio mara ya kwanza kwa Spika Makinda kuonya tabia hizo za wabunge.

No comments:

 

ADVERTISE WITH US

AFRICAN FASHION

PLACE YOUR ADS HERE!